Thursday, December 18, 2014

Robert Alai



Tweets zilizonukuliwa hapo juu na chini ndizo zilizomfikisha kortini mwanablogu maarufu na mwenye utata wa Kenya kwa madai kuwa amemdhalilisha rais.



Siku hiyo aliyomwita rais jina hilo, pia akaweka namba za simu za rais na baadhi ya maafisa waandamizi.

Robert Alai, mkosoaji mkali wa serikali, alikana mashtaka hayo na kuachiwa kwa dhamana kwa dola za Kimarekani $2,000 na kuamriwa kutokuweka ujumbe unaofanana na huo wakati uchunguzi ukiendelea.


Bw Alai ni miongoni mwa wanablogu maarufu na wenye ushawishi mkubwa Kenya akiwa na wafuasi 140,000 kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Bw Alai tayari ana wengi wanaomwuunga mkono kwenye mtandao wa kijami wa Twitter kutoka kwa Wakenya wanaoona mashtaka hayo kama mbinu ya serikali ya kuzuia uhuru wa vyombo vya habari.

 Alipotolewa tu kwa dhamana, aliandika kwenye Twitter kuwa itakuwa ngumu kumnyamazisha.

Miaka miwili ilyopita, alikamatwa na kuhojiwa baada ya kudai kuwa msemaji wa serikali ya wakati huo alikuwa akipanga kumwuua.

0 TOA MAONI YAKO HAPA.:

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!