Wednesday, May 7, 2014

Liu Fenghe akiwa hospitali na nondo kichwani.

FUNDI majengo Liu Fenghe wa nchini China, amenusurika kifo baada ya kuchomwa na nondo kichwani na kuzama inchi 8 ambazo ni sawa na sentimita 20.
 



Liu alikuwa akiongea na rafiki yake na kwa bahati mbaya alidondokewa na nondo iliyomchoma kichwani.
 
Rafiki yake Liu aitwaye Zhang anasema:

"Ilikuwa ghafla. Kabla sijafanya chochote Liu alikuwa katika dimbwi la damu."Inadhaniwa kuwa chuma hicho kilidondoka kutoka ghorofa ya 25 ya jengo walilokuwemo mafundi hao mpaka kusababisha maafa hayo.
 

 Picha ya X-ray ikionyesha jinsi nondo hiyo ilivyoingia kichwani mwa bwana Liu.

Madaktari walimfanyia upasuaji wa haraka katika hospitali iliyopo jimbo la Shanghe nchini China na kueleza kuwa Liu hayupo tena katika hatari japo bado haijajulikana ni lini ataweza kurudi kazini.

posted by paparazi
 
 

0 TOA MAONI YAKO HAPA.:

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!